Wednesday, November 14, 2012

MASANJA alikua anaumwa sana na alilazwa hospitali ya BUGANDO,sasa cku 1 rafiki yake YUSUPH akaja kumjulia hali, alipofika akamkuta mgonjwa MASANJA anakunywa UJI, mambo yakawa hivi...

YUSUPH-pole sana rafiki angu!

MASANJA-(kwa lafudhi ya kisukuwa)asante bwana!

YUSUPH-usijali mungu atajalia utapona!

MASANJA-kweli ntaponaga kabisa!

huku akiendelea kunywa uji bwana MASANJA akaropoka...

MASANJA-ila kusema ukweli naumwaga! yaani naumwaga kweli!

YUSUPH-eh! unasema?

MASANJA-sio siri naumwaga yaani naumwag....

kabla hajamalizia bwana YUSUPH akadakia 'eh! naomba usiumwage kama umeushindwa huo UJI nipe mie nimalizie'

hahahaha kumbe MASANJA aliposema NAUMWAGA maana ake NAUMWA ila kwa SWAGA za KISUKUMA ndo lazima uweke GA! hahahaha haya twende NAWAPENDAGA!

CHEZEA MKE WA MTU WEWE